Monday, April 25, 2011

Maadhimisho miaka 47 Muungano kesho



MAADHIMISHO miaka 47 ya Sikukuu ya Muungano wa Tanzania yanatarajiwa kufanyika kesho huko visiwani Zanzibar
Katika taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu imesema kuwa, maadhimisho hayo kitaifa yanatarajiwa kufanyika katika Uwanja wa Amani kisiwani Zanzibar

Maadhimisho hayo ni kumbukumbu ya kukumbuka kuungana kwa nchi mbili ambazo ni Tanganyika na Zanzibar na kupatikana Tanzania nchi zilizoungana April 26, mwaka 1964 kwa kuchanganya udongo wa pande zote mbili na waasisi wa nchi hizo.

Hivyo kila mwaka ifikapo Aprili 26 ni siku ya mapumnziko kupisha sikukuu ya kumbukumbu hizo.

Hivyo watanzania wametakiwa kujitokeza kwa wingi uwanjani hapo kusherehekea kwa pamoja sikukuu hizo na milango ya uwanja huo ityafunguliwa kuanzia majira ya 12 asubuhi kuruhusu wananchi kujumuika katika sherehe hizo

No comments:

Post a Comment